Habari
SIMBACHAWENE AIPONGEZA TBA: UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJENGO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene ameipongeza Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Ujenzi na usimamizi wa majengo ya Serikali ikiwemo ujenzi wa Jengo la Ofisi hiyo, Mtumba jijini Dodoma.
Pongezi hizo amezitoa leo Juni 17, 2025 wakati akizindua maonesho ya wiki ya utumishi wa Umma yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Chinangali Park mkoani Dodoma ambayo yanaongozwa na kauli mbiu inayosema "Himiza matumizi ya mifumo ya kidijitali ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji".
Mhe.Simbachawene amesema matumizi ya mifumo ya kidigitali yamerahisisha shughuli mbalimbali za kiserikali ikiwemo kutoa nafasi za ajira pia imeongeza ufanisi na uwajibikaji wa kazi kwenye utumish wa Umma.
Ametoa wito kwa watumishi wote wa wizara na taasisi za umma kutumia TEHAMA ili kuwezesha wananchi kupata taarifa kwa urahisi na haraka