Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila katika hafla ya ufunguzi wa jengo la makazi ya watumishi wa umma la Magomeni Kota Awamu ya Pili B la ghorofa saba uliotekelezwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) lililopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Mkoani Dar es Salaam, tarehe 23 Julai, 2024.
Muonekano wa jengo la makazi ya watumishi wa umma la Magomeni Kota Awamu ya Pili B la ghorofa saba uliotekelezwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Mkoani Dar es Salaam lililogharimu Shilingi Bilioni 5.687.
Muonekano wa barabara ya Kaengesa - Chitete (km 6.4) sehemu ya Kaengesa Seminari ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameiwekea jiwe la msingi la ujenzi wa barabara hiyo leo tarehe 17 Julai, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa katika mkutano wa hadhara wa Wananchi katika uwanja wa CCM Mandela-Sumbawanga Mkoani Rukwa, leo tarehe 16 Julai 2024
Muonekano wa sehemu ya barabara ya Sumbawanga – Matai – Kasanga Port (km 107), iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami na kufunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa, tarehe 16 Julai, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa pamoja na viongozi wengine wa Serikali akikata utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya Sumbawanga – Matai – Kasanga Port (km 107) kwa kiwango cha lami Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa, tarehe 16 Julai, 2024.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akizungumza na kutoa maelekezo kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta baada ya kukagua mpasuko wa ardhi na kuporomoka kwa tuta la barabara katika eneo la Busunzu katika barabara ya Mvugwe – Makutano ya Nduta (km 59.35) iliyojengwa kwa kiwango cha lami, Wilaya Kibondo Mkoani Kigoma. Tarehe 10 Julai 2024.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango akitoa maelekezo kwa Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa na Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Mohamed Besta mara baada ya kupata maelezo ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Malagarasi - Ilunde - Uvinza (km 51.1) kwa kiwango cha lami katika Kambi ya Mkandarasi Kijiji cha Chakulu Wilayani Uvinza, leo tarehe 08 Julai 2024.
Muonekano wa Daraja la J.P. Magufuli (Kigongo – Busisi) lenye urefu wa Kilomita 3.0 na barabara unganishi Kilomita 1.66 linatarajiwa kuanza kutumika Tarehe 30 Disemba 2024.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akifafanua jambo wakati akichangia Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Bungeni jijini Dodoma, Tarehe 26 Juni, 2024.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akizungumza na Wabunge Wanawake wenye Majimbo katika kikao kilichofanyika Bungeni Juni 24, 2024, jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Kigoma, Eng. Narcis Choma (Wapili kushoto mbele), alipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Kabingo - Kasulu – Manyovu (Km 260) sehemu ya Mvugwe – Nduta (Km 59.35), mkoani humo.
Muonekano wa daraja la Malagarasi lenye urefu wa mita 77, mkoani Kigoma. Daraja hilo limejengwa na mkandarasi STECOL na limekamilika kwa asilimia 100.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya akitoa maelekezo kwa Meneja Mradi kutoka Kampuni ya kikandarasi ya STECOL, Cao XiaoJun (WaKwanza kulia) alipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Malagarasi-Ilunde – Uvinza (Km 51.1), mkoani Kigoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya wakifuatilia michango ya Wabunge wakati wa Bunge likijadili Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa Mwaka wa Fedha 2024/25, leo Tarehe 29 Mei 2024.
waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa Fedha 2024/2025 Bungeni , jijini Dodoma Mei 29, 2024
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akiwa katika Mohojiano na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Wakati wa Maonesho ya Sekta ya Ujenzi Bungeni jijini Dodoma, Mei 28 2024
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya (WaTatu kushoto waliokaa) na viongozi wa Umoja wa Wahandisi Washauri Barani Africa (FIDIC AFRICA), katika Mkutano wa 30 wa Wahandisi Washauri hao , jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi, (kulia) akiwa na Profesa maarufu nchini Kenya, Patrick Lumumba (kushoto) katika Mkutano wa 30 wa Wahandisi Washauri Barani Africa (FIDIC AFRICA), jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya akisisitiza jambo kwa Mhandisi wa Barabara, kutoka Kampuni ya Kikandarasi ya Reynolds kutoka Nigeria,Thobias Ngise (Wapili kushoto) wakati akikagua mradi wa ujenzi wa barabaara ya Mikumi - Kidatu- Ifakara sehemu ya Kidatu - Ifakara (Km 66.9) kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi wa Daraja la Ruaha Mkuu, mkoani Morogoro.
Kazi za urejeshaji wa mawasiliano ya barabara katika daraja la Mto Fulua, Wilayani Malinyi, mkoani Morogoro zikiendelea.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi, Godfrey Kasekenya akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Morogoro, Mhandisi, Alinanuswe Kyamba (kushoto) wakati akikagua daraja la Mto Namuhanga lililoathiriwa na mafuriko kutokana na mvua za El-Nino zilizonyesha mwaka huu, wilayani Ulanga, mkoani Morogoro.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akishuhudia wahandisi 48 wakila kiapo katika Mkutano wa Sita wa Mafundi Sanifu Tanzania wa mwaka 2024 uliofanyika jijini Dodoma. Mkutano huo umehudhuriwa na Mafundi Sanifu 800 kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akizungumza jambo katika Mkutano wa Sita wa Mafundi Sanifu Tanzania wa mwaka 2024, uliofanyika jijini Dodoma Mei 23, 2024.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akimkabidhi zawadi ya picha ya ukutani Balozi wa China nchini Tanzania, Chen Mingjian mara baada ya kufanya mazungumzo kuhusu ushirikiano wa masuala mbalimbali katika Sekta ya Ujenzi baina ya nchi hizo mbili, jijini Dar es Salaam Mei 20, 2024.