Kazi ya ujenzi wa barabara ya Kabingo-Kasulu-Manyovu KM 260.6 kwa kiwango cha lami ikiendelea mkoani Kigoma.
Muonekano wa daraja la Malagarasi linalojengwa sehemu ya Mvugwe-Nduta katika barabara ya Kabingo-Kasulu-Manyovu KM 260.6
Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya akikagua daraja la Malagarasi linalojengwa sehemu ya Mvugwe-Nduta ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 96, katika barabara ya Kabingo-Kasulu-Manyovu KM 260.6 mkoani Kigoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya akikagua daraja la Malagarasi linalojengwa sehemu ya Mvugwe-Nduta ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 96, katika barabara ya Kabingo-Kasulu-Manyovu KM 260.6 mkoani Kigoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya akikagua umadhubuti wa lami kwa kifaa maalum katika barabara ya Kabingo-Kasulu-Manyovu KM 260.6 ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami unaendelea mkoani Kigoma.
Mhandisi Mshauri kutoka Kampuni ya Beza/Afrisa Eng. Shegaw Berhanie (kulia), akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, kuhusu mchoro wa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato wakati Waziri huyo alipotembelea na kukagua maendeleo yake Septemba 29, 2023, jijini Dodoma.
Muonekano wa jengo la abiria litakavyokuwa katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato mara baada ya kukamilika ujenzi wake, jijini Dodoma. Jengo hilo litakuwa na uwezo wa kupokea abiria Milioni 1.5 kwa mwaka na abiria 800 kwa wakati mmoja.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akitoa maelekezo kwa mkandarasi wa Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group wakati alipokagua maendeleo ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, Septemba 29, 2023 jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akizunguma na menejimenti ya Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB), mara baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Bodi hiyo iliyo chini ya Wizara ya Ujenzi, jijini Dodoma Septemba 27, 2023
Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya akisisitiza jambo kwa Mbunge wa Urambo Mhe. Margareth Sitta alipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Tabora- Kigoma sehemu ya Urambo round about.
Muonekano wa barabara ya Tabora-Kigoma sehemu ya Kazilambwa-Chagu yenye urefu wa KM 36 ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 99.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, katika picha ya pamoja na menejimenti za Taasisi za Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) katika kikao kazi cha uwasilishwaji wa taarifa za majukumu ya Taasisi hizo kilichofanyika jijini Dodoma Septemba 26, 2023.
Sehemu ya Menejimenti za Taasisi za Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majego na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa (hayupo pichani), katika kikao kazi cha uwasilishwaji wa taarifa za majukumu ya Taasisi hizo kilichofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent L. Bashungwa, akizungumza na menejimenti za Taasisi za Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) na Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) katika kikao kazi cha uwasilishwaji wa taarifa za majukumu ya Taasisi hizo kilichofanyika jijini Dodoma Septemba 26, 2023. Katika kikao hicho Waziri Bashungwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Eng. Aisha Amour na sehemu ya Menejimenti ya Wizara.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akiteta jambo na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel, katika mkutano wa hadhara wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na wananchi uliofanyika katika Uwanja wa Mitwero mkoani Lindi tarehe 19 Septemba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa na viongozi wengi akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Nachingwea – Ruangwa, sehemu ya Ruangwa – Nanganga (km 53.2) inayojengwa kwa kiwango cha lami, leo tarehe 18 Septemba 2023
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Nachingwea – Ruangwa, sehemu ya Ruangwa – Nanganga (km 53.2) inayojengwa kwa kiwango cha lami, leo tarehe 18 Septemba 2023.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa na viongozi wengine wakati akiwasili katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Nachingwea – Ruangwa, sehemu ya Ruangwa – Nanganga (km 53.2) inayojengwa kwa kiwango cha lami, leo tarehe 18 Septemba 2023. Mgeni Rasmi katika hafla hiyo ni Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Eng. Aisha Amour, akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Frank Chonya, mara walipotembelea Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Majaliwa uliopo Wilayani humo mkoani Lindi, Septemba 17, 2023. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Mohamed Besta.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Eng. Aisha Amour pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Eng. Mohamed Besta, wakati wakikagua maandalizi ya sherehe ya uwekaji jiwe la Msingi wa barabara ya Ruangwa - Nanganga (km 53 5), utakaofanyika Septemba 18, 2023 katika kijiji cha Nandagala mkoani Lindi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Eng. Aisha Amour akitoa maelekezo wakati akikagua maandalizi ya uwekaji jiwe la msingi wa barabara ya Ruangwa - Nanganga (km 53 5), utakaofanyika Septemba 18, 2023 katika kijiji cha Nandagala mkoani Lindi.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa (katikati), akisikiliza kwa makini hoja za wananchi wakati wa Ziara ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Mtwara ikiwa ni siku ya pili katika mkoa huo ambapo amekagua miradi mbalimbali na kuzungumza na wananchi katika Halmashauri ya Nanyamba pamoja na Newala.
Naibu Waziri Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya (kushoto), akiwa Kwenye mkutano wa nne wa Mawaziri wa Masuala ya Uchukuzi, Miundombinu na Nishati wa Bara la Afrika uliofanyika kuanzia tarehe 12 -15 SEPTEMBA, 2023 Zanzibar ambapo nchi 41 kati ya 55 zimeshiriki katika mkutano huo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi (hawapo pichani), waliofika kushuhudia uwekaji wa Jiwe la msingi la Ufunguzi wa Barabara ya Mtwara - Newala - Masasi, sehemu ya Mtwara - Mnivata yenye urefu wa kilometa 50 iliyogharamiwa na Serikali kwa 100% kwa gharama ya jumla ya Shilingi Bilioni 93.83, tarehe 14 Septemba 2023, mkoani Mtwara,
Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa, akizungumza na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, mkoani Mtwara.