Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Chama cha Wabunifu Majengo Tanzania (AAT), mara baada ya kufungua mkutano wao wa 27 na Kumbukizi ya miaka 40 ya Chama hicho uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi, akitoa cheti kwa mmoja wa wanafunzi walioshiriki katika mkutano wa 27 na Kumbukizi ya miaka 40 ya Chama cha Wabunifu Majengo Tanzania (AAT), uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akifafanua jambo katika hafla ya ufunguzi wa mkutano wa 27 na Kumbukizi ya miaka 40 ya Chama cha Wabunifu Majengo Tanzania (AAT), uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu Wizara Ya Ujenzi, Bw. Ludovick Nduhiye (wa tatu kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya ukaguzi kutoka Wizara ya Ujenzi, mara baada ya kufunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wajumbe hao yaliyofanyika Jijini Mwanza.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, BW. Ludovick Nduhiye akitoa vyeti kwa baadhi ya wajumbe wa kamati ya ukaguzi ya Ujenzi walioshiriki katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika jijini Mwanza.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, BW. Ludovick Nduhiye akitoa vyeti kwa baadhi ya wajumbe wa kamati ya ukaguzi ya Ujenzi walioshiriki katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika jijini Mwanza.
Mratibu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa wanawake katika kazi za barabara Eng. Gladness Kitaly, akikabidhi vifaa vya kujifunzia kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Wasioona ya Buigiri, Samuel Jonathan, wakati Ujumbe wa Wahandisi kutoka Wizara ya Ujenzi ulipofika Shuleni hapo kuhamasisha masomo ya Sayansi na Hisabati kwa wanafunzi hao, wilayani Chamwino, jijini Dodoma.
Mratibu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa wanawake katika kazi za barabara Eng. Gladness Kitaly, akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Wasioona ya Buigiri, wilayani Chamwino, jijini Dodoma wakati Ujumbe wa Wahandisi kutoka Wizara ya Ujenzi ulipofika Shuleni hapo kuhamasisha masomo ya Sayansi na Hisabati kwa wanafunzi hao.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akikagua atahari za mvua katika mji wa Hedaru na Saweni, wilayani Same, Mkoani Kilimanjaro, tarehe 24 Novemba, 2023.
Mwezeshaji kutoka Uptake Business Resources, CPA Peter Mwambuja, akielezea mada mbalimbali kwa wajumbe wa kamati ya ukaguzi kutoka Wizara ya ujenzi kwa lengo la kuwajengea uwezo, jijini Mwanza.
Mkurugenzi wa Barabara kutoka Wizara ya Ujenzi, Eng. Aloyce Matei (kulia), akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, wakati alipokagua ujenzi wa barabara ya Mkange - Tungamaa- Pangani (Km 120.8), wilayani Pangani, mkoani Tanga.
Wajumbe wa Kamati ya Ukaguzi kutoka Wizara ya Ujenzi wakikagua na kutembelea utekelezaji wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa umma katika eneo Ghana, jijini Mwanza.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar na wataalam kutoka Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi (SMZ), wakati walipotembelea mradi wa ujenzi wa Miundombinu ya Usafiri wa Haraka wa Mabasi (BRT), Awamu ya Tatu Jijini Dar es Salaam
Baadhi ya Makandarasi na wadau wa Sekta ya Ujenzi wakiwa katika Mkutano wa Mashauriano kati ya Serikali na Makandarasi wazawa, Washauri elekezi pamoja na wadau mbalimbali wa Sekta ya Ujenzi kujadili nafasi yao katika utekelezaji wa miradi na masuala yanayohusu Sekta ya Ujenzi, terehe 21 Novemba, 2023 jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akizungumza na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo katika Mkutano wa Mashauriano kati ya Serikali na Makandarasi wazawa, Washauri elekezi pamoja na wadau mbalimbali wa Sekta ya Ujenzi kujadili nafasi yao katika utekelezaji wa miradi na masuala yanayohusu Sekta ya Ujenzi, terehe 21 Novemba, 2023 jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Mashauriano kati ya Serikali na Makandarasi wazawa, Washauri elekezi pamoja na wadau mbalimbali wa Sekta ya Ujenzi kujadili nafasi yao katika utekelezaji wa miradi na masuala yanayohusu Sekta ya Ujenzi, terehe 21 Novemba, 2023 jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akizungumza na Watumishi wa Wizara hiyo (hawapo pichani), wakati alipokutana nao katika kikao kazi kilichofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa (katikati), Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya (kulia) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Ludovick Nduhiye (kushoto), wakipitia baadhi ya hoja za watumishi zilizowasilishwa kwa njia ya maandishi katika kikao kazi kilichofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Wizara hiyo mara baada ya kumaliza kikao kazi na watumishi wa Wizara, jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa (kulia), akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Eng. Aisha Amour (kushoto), wakati wa kikao cha Mameneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), wa mikoa yote nchini kilichofanyika jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Mkutano wa Ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SJMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuhusu Sekta ya Ujenzi ambaye ni Waziri wa Ujenzi SJMT, Innocent Bashungwa, akifungua Mkutano wa Sita wa Ushirikiano kati ya SJMT na SMZ kuhusu Sekta ya Ujenzi, uliofanyika tarehe 11 Novemba, 2023, jijini Mwanza.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanyika Novemba 08, 2023 Jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanyika Novemba 08, 2023 Jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akikabidhi vitendea kazi kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Mhandisi Deogratias Nyanda wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanyika Novemba 08 ,2023 Jijini Dodoma.
16th Joint Transport Sector Review meeting.