Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Ujenzi

Habari

Kasekenya amtaka mkandarasi Daraja la JPM kufidia muda ulipotea


Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amemtaka mkandarasi wa kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation na China Railway 15 Bureau Group Corporation wanaojenga Daraja la JPM (Kigongo hadi Busisi), lenye urefu wa kilometa 3.2 kufidia muda uliopotea na kuwafanya wawe nyuma kwa asilimia 7.

Akikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa daraja hilo linalounganisha wilaya za Misungwi na Sengerema jijini Mwanza, Naibu Waziri Kasekenya amebaini kuwepo kwa ucheleweshwaji wa mradi huo kutokana na changamoto mbalimbali ambapo kwa sasa mradi umefikia asilimia 29 huku mpango kazi wa ujenzi wake ukiitaka kazi hiyo kuwa imefikia asilimia 36.

“Hakikisheni mnafidia muda uliopotea kwa kuongeza nguvu kazi au vitendea kazi na ikiwezekana mfanye kazi ya ujenzi wa daraja hili usiku na mchana ili kuhakikisha daraja hili si tu linakamilika ndani ya miezi 48, lakini pia linakamilika kwa viwango vilivyo ainishwa kwenye mkataba ili liweze kudumu kwa miaka 120 kama ilivyokusudiwa”, amesema Mhandisi Kasekenya.

Ameongeza kuwa ujenzi wa Daraja la JPM (Kigongo - Busisi), ukikamilika unatarajiwa kuibua fursa za biashara na kiuchumi kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza, mikoa jirani ya Kanda ya Ziwa lakini pia nchi jirani za Rwanda, Uganda na Burundi.

Naibu Waziri huyo amewataka watanzania kutembea kifua mbele na kujivunia mradi huo mkubwa unaotelekezwa kwa fedha za Serikali ya Tanzania, yaani fedha halali ya walipakodi, ambapo kwa sasa tayari umetoa ajira kwa idadi kubwa ya watanzania na kuwapa fursa za kibiashara wananchi wa maeneo ya jirani na mradi huo.

Aidha, Mhandisi Kasekenya amempongeza Rais wa Jamhuri y