Habari
UJENZI KIWANJA CHA NDEGE CHA ARUSHA WATAJWA KUTATUA CHANGAMOTO

Naibu Waziri Mwakibete amesema pamoja na maboresho hayo Serikali ina mpango wa kukiwekea taa kiwanja hicho ili kukiwezesha kuhudumia watalii na wasafiri wengine kwa saa 24.
Kwa upande wake Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Arusha Mhandisi Elipid Tesha, amesema maboresho yaliyoanza kufanywa kiwanjani hapo ni pamoja na barabara ya kuruka na kutua ndege, maegesho ya ndege, eneo la kuegesha magari ambapo kumeongeza miruko ya ndege kutoka 8,271 kwa mwaka 2020 mpaka 14,244 kwa mwaka 2022 huku likitajwa kuwa ni ongezeko la asilimia 41.
Mhandisi Tesha ameongeza kuwa pamoja na ongezeko la miruko kiwanjani hapo, pia mapato yameongezeka kutoka milioni zaidi ya 900 kwa mwaka 2021 mpaka kufikia bilioni moja nukta 2 mwaka 2022 hivyo kukifanya kiwanja hicho kuvuka lengo la ukusanyaji.
Naibu Waziri yuko Mkoani Arusha kukagua miradi na kutembelea taasisi kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa na sekta ya Uchukuzi.