Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Ujenzi

Habari

KUSUASUA KWA MRADI KASEKENYA ATOA MAELEKEZO


Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya ameeleza kutoridhishwa  na kasi ya ujenzi wa Barabara ya Malagarasi _Ilunde_Uvinza (51.1km)inayojengwa kwa kiwango cha lami Mkoani Kigoma.

Kasekenya , Ameyasema hayo wakati alipokagua mradi huo unaojengwa na Mkandarasi STECOL COOPERATION ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 45 mpaka sasa na unatakiwa kukamilika Januari  2024.

“Barabara hii ni muhimu  inaunganisha nchi za jirani kama  Congo,Rwanda na Burundi vile vile wananchi wanahitaji barabara hii kwa ajili ya shughuli zao za kiuchumi na biashara hivyo kutokukamilika kwake kwa wakati kunachelewesha maendeleo ya wananchi" amesema Kasekenya

Aidha, ameongeza kwa kumtaka Mhandisi Mshauri  kuhakikisha Mkandarasi anaongeza nguvu  kazi kwenye mradi pamoja na kuongeza vifaa,wafanyakazi na masaa ya kazi ya ziada Vilevile, Mkandarasi ajue  sababu zinazokwamisha mradi ili zitatuliwe na mradi  kumalizika kwa wakati.

Kwa upande wake Meneja  wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Narcis Choma,  amemhakikishia Naibu Waziri Kasekenya kusimamia mradi kwa ukaribu na kuhakikisha unamalizika kwa wakati uliopangwa.