Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Karim Mkorehe akiwa na Watumishi wa Wizara ya Ujenzi, mara baada ya kufunga mafunzo jumuishi katika kuboresha Utendaji kazi wa watumishi hao yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Afya (CEDHA), jijini Arusha.
Watumishi wa Wizara ya Ujenzi, wakiwa katika mafunzo jumuishi katika kuboresha Utendaji kazi wa watumishi hao yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Afya (CEDHA), jijini Arusha.
Muonekano wa Jengo la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato, jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega akiangalia tuzo aliyopewa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), katika maadhimisho ya 22 ya Siku ya Wahandisi Tanzania, yaliyofanyika Septemba 26, 2025 jijini Dar es Salaam.
Viongozi wa Wizara ya Ujenzi na waalikwa mbalimbali wakiwa katika maadhimisho ya 22 ya Siku ya Wahandisi Tanzania yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, Septemba 25, 2025
Wahandisi wakila kiapo cha utiifu katika maadhimisho ya 22 ya Siku ya Wahandisi Tanzania yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, Septemba 25, 2025
Maboresho ya Mfumo wa Usimamizi wa Kazi za Matengenezo (MUM)
Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Balozi, Mhandisi, Aisha Amour (waliokaa katikati) akiwa na wajumbe wa Mkutano wa 12 wa Baraza la Wafanyakazi la Bodi ya Usajili ya Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi, Mhandisi Aisha Amour, akiwa na wajumbe wa Menejimenti na Mameneja wa TANROADS wa mikoa, mara baada ya kufungua mafunzo ya Uongozi kwa viongozi hao, mkoani Morogoro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akifunua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Daraja la J.P Magufuli (Km 3) mkoani Mwanza Juni 19, 2025.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli akisaini kitabu cha Wageni alipotembelea banda la Wizara ya Ujenzi katika maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 19, 2025 Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Banda la Wizara ya Ujenzi Juni 18, 2025 katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025, Chinangali Park jijini Dodoma.
Watumishi wa Wizara ya Ujenzi wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara hiyo katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma. Maonesho hayo yanaongozwa na kaulimbiu "Himiza matumizi ya mifumo ya kidijitali ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji".
Wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi, Wakala ya Barabara (TANROADS) na wapandaji miti kutoka Jeshi la Kujenga Taifa -Makutupora wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukamilisha zoezi la upandaji miti 150 pembezoni mwa barabara ya mzunguko wa nje wa jiji la Dodoma kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani 2025.
Wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi, Wakala ya Barabara (TANROADS) na wapandaji miti kutoka Jeshi la Kujenga Taifa -Makutupora wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukamilisha zoezi la upandaji miti 150 pembezoni mwa barabara ya mzunguko wa nje wa jiji la Dodoma kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani 2025.
Mhandisi Mkuu, Chacha Harun kutoka Kitengo cha Usalama na Mazingira, Wizara ya Ujenzi akitoa elimu kwa sehemu ya Menejimenti ya Wizara hiyo ilipotembelea na kukagua banda la Wizara ya Ujenzi na Wakala ya barabara (TANROADS), leo Juni 3, 2025 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre, jijini Dodoma yanapofanyika maonesho ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani 2025.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi, Godfrey Kasekenya akimpa zawadi Makamu wa Waziri wa Ardhi, Miundombinu na Usafirishaji wa Jamhuri ya Korea, Mhe. Hyun Hwan Jin mara baada ya kumaliza kikao chao kilichofanyika katika Ofisi za Wizara hiyo jijini Dodoma leo, Mei 27, 2025
Muonekano wa sehemu ya barabara ya mzunguko wa nje ya Dodoma (Dodoma Outer Ring Road) ambayo kwa sasa utekelezaji wake umefika zaidi ya asilimia 85.
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, kutoka Wizara ya Ujenzi, Bw. Mrisho Mrisho (katikati mbele) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi hodari pamoja na wawakilishi wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo mara baada ya kugawa zawadi ya vyeti na fedha taslimu kwa watumishi Hodari wa Idara na Vitengo kwa mwaka wa Fedha 2024/2025 leo, Mei 20,2025 jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amepokea Taarifa ya Kamati ya uchunguzi ya Kivuko cha MV. Tanga kinachotoa huduma wilayani Pangani, Mkoani Tanga leo Mei 20, 2025 Ofisini kwake jijini Dodoma. Kamati hiyo aliiunda Mei 13, 2025 alipofanya ziara mkoani Tanga na kuipa siku Saba kuchunguza changamoto zinazojitokeza mara kwa mara katika kivuko hicho baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kuhusu kusuasua kwa utendaji wake.
Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala leo, tarehe 20 Mei, 2025 Ofisini kwake, jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma leo, Mei 05, 2025 wakati wa uwasilishaji wa hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Balozi, Mhandisi Aisha Amour akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma leo, Mei 05, 2025 wakati wa uwasilishaji wa hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi, Godfrey Kasekenya (kulia) akimpongeza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega mara baada ya kuwasilisha Bungeni Mpango na makadirio ya Mapato na Matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2025/2026 leo tarehe 05 Mei, 2025 mkoani Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega akiwasilisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2025/ 2026, Bungeni jijini Dodoma leo Mei 05, 2025. Waziri huyo ameomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi Trilioni 2.28 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
